
Mbao FC
GF Trucks na Mbao walisaini mkataba wa miaka mitatu ambapo sasa umebaki mwaka mmoja ambao wanaendelea nao huku ukiwa umeboreshwa lakini hawakuweza wazi maboresho hayo.
Mtendaji Mkuu wa GF Trucks, Imrani Karmali amesema bado wana imani na mahusiano mazuri na timu hiyo licha ya kukiri kuwa msimu uliopita haukuwa mzuri kwao.
Nae Mwenyekiti wa Mbao, Solly Njashi ameishukuru kampuni hiyo kwa kuendelea kuwaamini huku akiwahikishia kufanya maboresho kwenye kikosi ili kuongeza ushindani kwenye ligi.