
Nembo ya shirikisho la soka nchini TFF
Katika salam zake, TFF inawapa pole familia ya marehemu, ndugu, jamaa, marafiki na kusema kwa niaba ya familia ya mpira wa miguu nchini, wako pamoja katika kipindi hiki cha maombolezo.
Marehemu Willie Chiwango ni miongoni mwa waandishi wa habari wa michezo wakongwe kabisa, aliambatana na timu ya taifa ‘Taifa Stars’ iliyoshiriki michuano ya Mataifa Afrika mwaka 1980 nchini Nigeria.
TFF ilimpa cheti cha heshima marehemu Chiwango katika zoezi la kuwakumbuka na kutambua mchango wa viongozi, wachezaji, waandishi wa habari za michezo waliojitoa katika sekta ya mpira wa miguu nchini.