Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Simba yatuma salamu kwa Yanga

Saturday , 21st Oct , 2017

Klabu ya soka ya Simba imeendelea kuongoza msimamo wa ligi kuu soka Tanzania Bara baada ya kufanikiwa kuiadhibu Njombe Mji mabao 4-0 kwenye mchezo wa raundi ya 7 uliomalizika jioni hii kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

Katika mchezo huo Simba ilianza kwa kushambulia lakini Njombe Mji walijitahidi kuwadhibiti washambuliaji wa Simba hadi dakika ya 28 ambapo mshambuliaji Emmanuel Okwi alifanikiwa kuiandikia Simba bao la kuongoza ambalo lilidumu hadi mapumziko.

Kipindi cha pili Simba walirejea kwa kasi na kuliandama lango la Njombe Mji ambapo katika dakika ya 51, kiungo Mzamiru Yassin alifanikiwa kufunga bao la pili kabla ya kuongeza bao la tatu dakika ya 52. Simba iliendelea kushambulia na kufunga bao la nne kupitia kwa Laudit Mavugo.

Simba sasa inaongoza ligi ikiwa na alama 15 sawa na Mtibwa Sugar ambayo nayo imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Tanzania Prisons. Azam FC imetoka sare ya 0-0 na Mbao FC wakati Lipuli FC imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Majimaji FC. Matokeo mengine Ndanda FC imetoka sare ya 0-0 dhidi ya Singida United.

Emmanuel Okwi sasa amefikisha mabao 8 akiwa anaongoza orodha ya wafungaji msimu huu. Baada ya mchezo wa leo Simba itaelekea visiwani Zanzibar kujiwinda na mchezo dhidi ya watani wao wa jadi Yanga wikiendi ijayo.

HABARI ZAIDI

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90