Thursday , 4th Aug , 2016

Huku kukiwa na taarifa za klabu ya Manchester United, kumalizana na Juventus, juu ya kiungo wa timu hiyo ya Italia, Paul Pogba, kocha wa United, Jose Mourinho amekataa kuweka wazi juu ya uhamisho huo.

Kocha wa Manchester United Jose Mourinho amekiri kuwa anataka kufunga usajili na mchezaji mmoja hivi karibuni, lakini akakataa kutaja jina la mchezaji huyo.

Mourinho, amesema dirisha la usajili linafungwa Agost 31, hivyo kuna muda wa kutosha kufanya usajili wa mwisho, ili kuwahi msimu mpya wa EPL.

Tunataka kusajili mchezaji mmoja, huo ndiyo ukweli."Sitaki kuzungumzia juu ya Paul Pogba, kwa sababu ni mchezaji wa Juventus, na sitaki makocha wengine wazungumzie wachezaji wangu. Amesema Mourinho.