Friday , 28th Mar , 2014

Katika masumbwi hii leo mabondia Thomas Mashali na Japhet Kaseba wamepima uzito na afya zao tayari kabisa kwa pambano lao la uzito wa light-heavy kilo 79 litalopigwa kesho kwenye ukumbi wa PTA jijini Dar es Salaam

Pambano hilo litasimamiwa na PST ambapo rais wake Emmanuel Mlundwa amewataka mabondia hao kucheza mchezo uzuri katika pambano hilo ambalo amesema litakua la raundi 10 kuwania mkanda wa kimataifa wa UBO Afrika

Nao mabondia hao Japhet Kaseba na Thomas Mashali ambao wamevuta hisia kwa mashabiki wao mara baada ya zoezi la upimaji uzito kila mmoja ameatamba kuibuka na ushindi na kuwataka mashabiki wao wasiwe na wasiwasi juu ya pambano hilo

Na katika kuhakikisha mpambano huo unakuwa na maamuzi ya haki na usawa katika maamuzi ya mapambano yote hapo kesho, Mratibu wa pambano hilo Ramadhan Mwazowa ametoa wito kwa majaji na waamuzi wa mchezo huo kuchezesha na kuwa na maamuzi yatakayozingatia sheria za mchezo huo

Mwazowa ameongeza kuwa uchezeshaji unaozingatia sheria na taratibu za mchezo huo kimataifa utafungua milango kwa waamuzi hao kupata michezo mingi ya kimataifa nje ya nchi.