Wednesday , 29th Jun , 2016

Kiungo Daniele de Rossi ataikosa mechi ya robo fainali ya michuano ya Euro 2016 baina ya timu yake ya Taifa ya Italia dhidi ya Ujerumani itakayopigwa Jumamosi hii.

Daniele de Rossi katika jezi ya taifa lake la Italia

De Rossi anayekipiga na AS Roma ya Italia alilazimika kuondoka uwanjani dakika ya 54 ya mchezo baada ya kuumia nyonga wakati timu yake ya taifa ikiwavua ubingwa Hispania kwa kuipa kipigo cha mabao mawili kwa sifuri.

Nafasi ya nyota huyo huenda ikachukuliwa na kiungo wa Juventus Giovanni Struaro ambaye inasemekana yupo tayari kwa ajili ya kuziba pengo hilo.

Kikosi cha Italia chini ya kocha Antonio Conte kimekuwa na matokeo mazuri katika hatua ya makundi ikifanikiwa kuzifunga Ubelgiji na Sweden .