
Kocha msaidizi wa Klabu hiyo Juma Mwambusi amesema, michuano hiyo itakifanya kikosi hicho kiwe na uzoefu zaidi kwani wanatarajia kutumia kikosi kipana katika michuano hiyo.
Mwambusi amesema, walikuwa wasishiriki mashindano hayo lakini iliwalazimu kutokana na baadhi ya timu shiriki za michuano hiyo ambazo zinatoka nje ya nchi ambazo kwa upande wao itakuwa kama mechi za kirafiki.
Mwambusi amesema, kikosi kinamajeruhi ambao ni Amis Tambwe, Mbuyu Twite na Simon Msuva ambao mpaka sasa wanaendelea na mazoezi madogomadogo ili