Akizungumza na East Africa Radio, Mkwasa amesema, kwa upande wa mchezaji Raia wa Sierra Leone Lansana Kamara ambaye yupo katika majaribio hawawezi kumpima kwa mazoezi kama anafaa lakini wanaamini watapata majibu katika mechi za majaribio.
Mkwasa amesema, wamejaribu kujenga ukakamavu na kukazania masuala ya kiufundi pamoja na kutengeneza mambo ya msingi katika mpira kwani lengo lao ni kufanya vizuri mwanzo mpaka mwisho katika mashindano mbalimbali.


