Monday , 4th Jul , 2016

Klabu ya soka Chelsea imeshamsajili mshambuliaji Michy Batshuayi kutoka katika klabu ya Marseille kwa mkataba wa miaka mitano.

Mshambuliaji huyo Mbelgiji mwenye umri wa miaka 22 anakuwa wa kwanza kununuliwa na meneja mpya pale Stamford Bridge.

Malipo ya mshambuliaji huyo hayajawekwa wazi lakini inaaminika kuwa ni pauni milioni 33 sawa na Euro milioni.

Michy alifunga mabao 23 akiwa Marseille msimu uliopita kutoka alipojiunga na klabu hiyo kutoka katika klabu ya Marseille mwaka 2014.

Chanzo BBC.