Monday , 24th Mar , 2014

Chama cha netball Tanzania CHANETA ambao ndio wenyeji wa michuano ya klabu bingwa ya netball kwa nchi za afrika mashariki inayoendelea katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam kimesema kuwa kimeridhika na hali inavyokwenda katika michuano hiyo

Makamu mwenyekiti wa CHANETA Zainab Mbilo amesema kuwa kitu kingine ambacho ni cha kupongezwa ni kwa kuongezeka kwa timu za wanaume katika michuano hiyo kwani awali kulikua na timu mbili pekee

Mbilo amesema kuwa msimu huu umekua wa neema kwao kama wenyeji kwani timu nane za wanaume zinashiriki michuano hiyo na zimeonyesha uwezo mkubwa na pia waamuzi nao amewapongeza kwa kuchezesha kwa kufuata sheria za mchezo huo kitu ambacho kimepelekea kutokuwepo kwa malalamiko makubwa juu ya maamuzi katika michezo iliyokwishachezwa.