Msanii wa kundi la Weusi Nikki wa Pili
Msanii huyo ameyasema hayo aliposhiriki katika kipindi cha EADRIVE kinachorushwa na kituo cha East Afrika Radio,ambapo ameshiriki kama mtangazaji mwenza katika kipindi hicho.
Akichangia mada kuhusu usafiri wa mabasi ya mwendo kasi jijini Dar es salaam ambapo kampuni inayosimamia mradi huo UDART imetangaza kwamba inatarajia kusitisha matumizi ya tiketi za karatasi ifikapo Julai 30 mwaka huu ambapo abiria watatakiwa kutumia tiketi.
UDART wamesema Mpango huo umewalenga watu wazima ambapo kila mmoja atalazimika kutumia kadi na sio tiketi kama ilivyo sasa na wanafunzi pekee ndiyo watatumia tiketi.
Akichangia mpango huo msanii Nikki wa Pili amesema lengo hil;o ni jema na kwa nchi zinazoendelea teknolojia inasaidia sana kupunguza rushwa na ukiritimba wa kutoa huduma kwa wananchi.



