Wednesday , 22nd Apr , 2015

Staa wa muziki Size 8 kutoka Kenya, ambaye yupo katika kipindi kigumu cha kuuguliwa na mama yake ambaye anahitaji kupandikizwa figo nyingine.

msanii wa nchini Kenya Size 8 akiwa na mama yake

Mwanadada huyo ameungwa mkono na msanii mwenzake Lady B kutoa wito kwa mashabiki kusaidia kupatikana kwa fedha za matibabu ya mzazi wake huyo.

Kwa njia ya mtandao, Lady B ameeleza kuwa, akiwa kama mama anaelewa kabisa uzito wa kuwa na mama mgonjwa, akiwataka wakenya kuungana kumsapoti Size 8 katika kipindi hiki cha majaribu kwake.

Kuuguliwa kwa msanii huyu, kumemfanya kusitisha shughuli zake za muziki kutoa nafasi ya kumhudumia mgonjwa ambaye matibabu yake yanahitaji gharama kubwa kufanyika, nchini India.