
Camp Mulla wakati wapo pamoja
Shappaman ameweka wazi kuwa, mgawanyiko wa kundi hilo ulikuwa hauna budi kutokana na wanakikundi Thee MC Africa maarufu kama Taio na Lady Karun ama Miss Karun kutakiwa kuwa katika ratiba nyingine nje ya nchi, kitu ambacho kilileta kikwazo kikubwa kwa wao kuendelea kama kundi.
Maelezo haya ya Shappaman yamekuja baada ya kuwepo kwa maswali mengi juu ya sababu hasa ambayo ilisababisha kundi hili kuizima nyota yao mara tu baada ya kuingia katika jukwaa la kimataifa la muziki.