
mwimbaji nyota wa taarab nchini Mzee Yusuf
Akiongea kwenye kipindi cha Tam Tam za Mwambao cha East Africa Radio, Mzee Yusuf amesema wimbo huo utakaokuwa ni zawadi pekee kwa mashabiki wake wa taarab utatoka hivi karibuni.
Amesema baada ya kutoa wimbo huo, ataacha kabisa kutoa nyimbo mpya, na badala yake atakuwa anawatungia nyimbo waimbaji wake, na yeye atakuwa akipanda kuimba nyimbo zake za zamani tu.
