Tuesday , 7th Feb , 2017

Rapa Nikki Mbishi amefunguka na kusema haamini kama kitengo cha kudhibiti dawa za kulevya hakijawahi kuwaona au kuwasikia watu wanaojihusisha na dawa hizo mpaka kufika hatua ya kuwakamata watu wadogo wadogo.

Nikki Mbishi

Akiongea na EATV Nikki Mbishi anadai kina Wema Sepetu, Mr Blue na wasanii wengine wengine waliotaja ni wadogo, tena watoto wadogo hata kwa umri kwani madawa yalikuwepo kabla yao na watu wametajirika na kupika pesa nyingi sana kupitia hayo hayo madude. 

Itazame hapa video nzima Nikki Mbishi akifunguka sakata hili la wasanii kukamatwa na kuhusishwa na matumizi ya dawa za kulevya.