Tuesday , 1st Jul , 2014

Msanii wa nchini Burundi anayeishi Kenya Jean Pierre Nimbona a.k.a Kidumu anatarajia kukonga nyoyo za mashabiki katika tamasha la muziki litakalofanyika tarehe 11 mwezi huu Jijini Kigali nchini Rwanda.

Mwanamuziki huyo nyota ambaye amekuwa akitumbuiza kwa kualikwa katika maonesho kadhaa nchini humo, ameweka wazi kuwa hivi sasa ameamua kuandaa tamasha lake binafsi ambalo atatambulisha nyimbo zake mpya.

Kidumu pia atashirikiana na msanii wa nchini Rwanda Alpha Rwirangira amabaye atakuwa mstari wa mbele katika kunogesha tamasha hilo kubwa.