Thursday , 1st May , 2014

Katika kuonesha kupanuka na kukua kwa soko la muziki hapa Tanzania, Mtayarishaji muziki John B kutoka Grandmasters Records Label ametangaza kupata mchongo na kampuni ya Foxfuse kutoka nchini Marekani.

John Blass

Mchongo huu utasaidia kuingiza muziki anaotengeneza katika soko la kimataifa kwa kuiuza kupitia mitandao maarufu kama Amazon na i-Tunes.

John B amesema kuwa, kazi rasmi na kampuni hii itaanza Tarehe 6 mwezi Mei, na hii itafaidisha kwa kiasi kikubwa wasanii kuingia katika jukwaa la kimataifa na kuuza kazi zao katika wigo mpana zaidi kupitia Grandmasters.

Kuhusiana na mchongo huu, hapa John B anafafanua zaidi.

Tags: