Monday , 21st Jul , 2014

Rapa maarufu Jay A wa nchini Kenya anatarajia kufanya kazi na wasanii wakubwa baada ya kula shavu la kufanya kazi na wasanii barani Afrika kupitia studio kubwa ya muziki nchini humo.

rapa Jay A wa nchini Kenya

Jay A anayetamba na wimbo wake 'Dumbala' remix akishirikisha wasanii DNA, Kenrazy, Sage na pia kuwahi kuimba pamoja na mwimbaji Nene wa Rwanda, ameelezea kuwa anatarajia kutoa kazi mpya na wasanii wakubwa wa kimataifa.

Hii itakuwa ni project yake kubwa kwa mkali huyo ambaye hakutaka kuwataja wasanii hao mpaka hapo mambo yakiwa yamekamilika.