
Iryn Namubiru
Iryn amesema kuwa, inasikitisha sana kuona kuwa anawekeza nguvu na pesa nyingi kutengeneza rekodi ambazo baada ya kukamilik, huchukuliwa na watu, kusambazwa na kutengenezewa remix za mixing zinazouzwa bila yeye kuona faida yoyote.
Iryn amesema kuwa, hiki ni kilio cha wasanii wengi, isipokuwa wanaogopa kusema kwa kuhofia kazi zao kuacha kupigwa , na amewataka wadau hawa wa muziki kufahamu juu ya kilio hiki na kuacha unyonyaji wanaofanya.