
Q Chillah
Akiongea kupitia eNewz ya EATV, baba mdogo wa Q Chila amesema kwamba hofu juu ya mkataba ni kwamba haukuwa na ushahidi wowote kwa upande wa Q Chilla hali inayombana na kushindwa kuendelea kimaisha na kushindwa kuwa na nyumba yake.
Amesema familia hiyo imeamua kumuandikia barua bosi wa Q Chillah ambaye ni QS Mhonda kumuomba kubadilisha sehemu mbalimbali ambazo zinambana sana kijana wao kiasi cha kumsababishia kurudi alipotoka jambo linaloweza kumvurugia maisha yake.
Tazama hapa alipokuwa akizungumza na eNewz