Tuesday , 10th Nov , 2015

Mwanamuziki Alicia Keys amefanikiwa kuchangisha dola milioni 3.8 - zaidi ya shilingi bilioni 8 za Tanzania katika tukio la hisani la burudani la Keep The Child Alive Black Ball lenye lengo kuokoa watoto dhidi ya janga la ugonjwa wa UKIMWI

BlackBall

Alicia kwa njia ya mtandao ameshukuru wote waliowezesha kufanikiwa kwa tukio hilo mwishoni mwa wiki, likishuhudia mahudhurio kutoka kwa mastaa wakubwa akiwepo Chris Rock aliyesherehesha, Lenny Kravitz, Wale kati ya wengine, akiwepo pia binti wa Rais Paul Kagame wa Rwanda, Angel Kagame.

Fedha ambazo zimepatikana katika shughuli hiyo zitatumika katika shughuli mbalimbali ambazo taasisi za Alicia zinashirikiana nazo kutoka mashirika yanayokabiliana na athari za gonjwa la UKIMWI kwa namna mbalimbali hususan kwa watoto katika bara la India na Afrika