
Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Glorious Luoga
Mkuu huyo wa wilaya hiyo ametoa agizo hilo wakati wa mkutano na watendaji wa mpaka wa silali na wafabiashara wa mahindi na kuongeza kuwa baada ya kikao hicho hataki kusikia ukiritimba huo unaendelea.
Hatua hiyo inakuja baada ya malalamiko ya wafabiashara kudai kuwa kuna baadhi ya watendaji wanawahangaisha wafanyabishara hao katika kutoa vibali na kupelekea usumbufu wa kuvusha au kuingiza bidhaa zao nchini.
Luoga amesisitiza watendaji watafute utaratibu mzuri ambao utaweza kuwapa urahisi wafanyabiashara wa pande zote mbili urahisi wa kufanya biashara zao ikiwemo na kuacha kutengeneza mazingira ya kutaka kupewa rushwa.