Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watatu wakamatwa na Jeshi la Polisi

Wednesday , 14th Feb , 2018

Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya limewakamata vijana watatu maeneo ya Mwanjelwa, Kata ya Ruanda Tarafa ya Iyunga Jijini Mbeya wakiwa na nyara za serikali ambazo ni vipande vinne vya meno ya Tembo.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoani humo DCP Mohammed Mpinga amesema mnamo Februari 05, 2018 majira ya 1:45 usiku walifanikiwa kuwakamata vijana hao waliotambulika kwa majina ya Kenedy Lupembe Simsokwe (43) ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha SAUT tawi la Mbeya na mkazi wa Iyela, Mathew Elikana Mwanjala (42) mpiga picha pamoja na Shaban Mkwiche (24) mkazi wa Iyunga.

Aidha, Kamanda Mpinga amesema baada ya kukamatwa na kupekuliwa watuhumiwa hao walikutwa na nyara hizo ambavyo vina uzito wa kilogram 5 vyenye thamani ya Tshs Milioni 33.

Kwa upande mwingine, DCP Mpinga amesema taratibu za kisheria zinafanyika ili watuhumiwa wafikishwe mahakamani kwa hatua zaidi, huku akiwataka wananchi kuacha tabia ya kuwa na tamaa ya kujipatia utajiri wa haraka kwa kutumia njia za mkato zisizo halali, badala yake wafanye kazi halali ili kupata kipato halali. 

HABARI ZAIDI

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90