Thursday , 14th Apr , 2016

Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili (WAWATA), umesema huenda juhudi za kukomesha mauaji ya vikongwe na watu wenye Albinism zisifanikiwe kutokana na baadhi ya wanasiasa kuingilia kati suala hilo.

Mratibu Mkuu wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania (Uwawata), Julius Juju (wapili kulia) akiwa na viongozi wengine wakimkabidhi Waziri wa Mambo ya Ndani ripoti yao

Imeelezwa kuwa licha ya juhudi zinazofanywa katika kukomesha mauaji hayo viongozi na wanasiasa wamekuwa ni mstari wa mbele kuwatetea watuhumiwa wa vitendo hivyo hatua ambayo inasababisha uendeshaji wa kesi kuwa mgumu.

Wakiongea baada ya kutembelea Shule ya Msingi Mitindo iliyopo wilayani Misungwi mkoani Mwanza Umoja huo umesema licha ya Changamto hiyo wanayokutana nayo lakini bado wanafanya juhudi za kupambana na hali hiyo kutokana na wengi wao kudaiwa kuhusika na suala hilo.

Shule ya Msingi Mitindo, Wilayani Misungwi Mkaoni Mwanza ina jumla ya wanafunzi 213, kati yao wenye ulemavu wa ngozi ni 87 idadi ambayo ni kubwa kuliko wanafunzi wenye mahitaji mengine.

Sauti ya Mmoja wa Viongozi wa UWAWATA waliotembelea shule ya msingi Mitindo ambapo anaeleza Jinsi wanasiasa wanavyochangia kuzuia mapambano dhidi ya mauaji ya Albino na Vikongwe