Mfano wa mwanamke akipima saratani ya matiti.
Akizungumza na katika hospitali ya Mloganzila leo Aprili 2, 2019 Daktari bingwa wa upasuaji wa matiti kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili , Gasper Haule amesema wanatarajia kufanya upasuaji kwa wagonjwa wanne wanaougua saratani hiyo mapema wiki hii.
“Tiba hii inafanywa kwa wale ambao wamegundulika kuwa saratani ipo katika hatua ya kwanza na ya pili, tutawafanyia upasuaji, tutatoa vivimbe na kisha watapewa tiba ya mionzi kwa kutumia mashine za kisasa zilizopo Ocean Road,” amesema Dkt. Haule.
Awali matibabu ya saratani ya matiti yalitolewa nchini kwa njia ya kuondoa kabisa titi katika hatua yoyote ya ugonjwa.




