
Mjumbe wa bunge maalumu la katiba Dkt Harrison Mwakyembe
Katika kikao cha Bunge cha majadiliano ya mapendekezo ya kamati kuhusu Sura Mbili za Rasimu ya katiba, Mwakyembe amesema kuwa, vijana wanaonukuu vitabu vyake hawanabudi kusoma kwa kina nakuelewa badala ya kukurupuka na kusoma mstari mmoja na kisha kuutumia.
Mwakyembe ameungana na wajumbe wenazake kutoka chama cha mapinduzi CCM kutaka muungano wa serikali mbili kwa madai kuwa serikali tatu zitasababisha mzigo wa gharama za uendeshaji kwa wananchi.