
Picha: Maktaba
Tukio hilo limetokea majira ya saa tano asubuhi wakati mtoto huyo akikatisha katika eneo la relini akitokea shuleni ndipo alipoigonga na kupoteza maisha papo hapo.
Mwenyekiti wa kitongoji hicho Hamrid Moses Kahemele amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba ametoa taarifa kituo cha Polisi Igurusi ili waufanyie uchunguzi mwili wa marehemu ndipo wakabidhiwe ndugu kwa ajili ya mazishi.
Kamanda wa polisi mkoani Mbeya Dhahiri Kidavashari alipotafutwa kuzungumzi tukio hilo hakupatikana kwani simu yake ya kinganjani iliita bila kupokelewa.