Mdee ametoa kauli yake hiyo kupitia mtandao wake wa kijamii wakati akiwashukuru wananchi na wadau waliopaza sauti kwa kitendo cha yeye kuwekwa chini ya ulinzi kwa zaidi ya muda uliopangwa.
"Kwa heshima kubwa niwashukuru sana wote mliopaza sauti zenu kutaka haki itendeke kwangu na kwa watoto wetu wa kike! Mapambano yanaendelea!" aliandika.
Halima Mdee aliwekwa chini ya ulinzi kwa agizo la mkuu wa wilaya ya Kinondoni Ally Happi kwa kuadai kwamba mbunge huyo alitoa maneno kukashifu na ya uchochezi katika mkutano wake wa Baraza la Wanawake CHADEMA uliofanyika katika ofisi za baraza hilo wakati akizungumza na wanahabari.



