Monday , 1st Feb , 2016

Jaji mkuu wa Tanzania Jaji Mohamed Chande Othman amesema kuwa mahakama itawachukulia hatua mahakimu wote walioshindwa kufikisha malengo ya mahakama walioshindwa kumaliza mashauri na kesi katika kiwango kilichowekwa na mahakama hiyo.

Akiongea na vyombo vya habari leo jijini Dar es salaam ,Jaji Chande amesema mahakama imeagiza majaji wafawidhi katika kila kanda kuangalia mahakimu zaidi ya 500 katika mahakama za wilaya na za mwanzo watoe maelezo kwa siku saba ili kila mmoja aeleze ni kwa nini hawajafikisha kiwango cha kumaliza kesi walizopangiwa kuzimaliza.

Jaji Chande amesema baada ya kujieleza watakaobainika kutokuwa na sababu ya kutosha watafunguliwa mashitaka ya kinidhamu za mahakama ili wachukuliwe hatua kutokana na kukiuka agizo la kuwataka kuwa na kiwango katika kuharakisha kumaliza mashauri.