Wednesday , 16th Sep , 2015

Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama barabarani limeanzisha mfumo wa kulipa faini kwa kutumia mfumo Wa kielectroniki ili kudhibiti vitendo vya rushwa na madereva wanaokimbia adhabu ili kudhibiti makosa mbalimbali ya barabarani

Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani Mohamed Mpinga

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salam Kamanda Mohamed Mpinga amesema mfumo huo ambao ni utekelezaji wa kanuni mpya za usalama barabarani utaanza kutumika kesho kwa jiji la Dar es salaam kwa majaribio na baadaye nchi nzima.

Kamanda Mpinga ameongeza kuwa mfumo huo utawezesha madereva waliokamatwa na makosa mbalimbali wata lipa kwa njia ya simu au kadi ya benki yoyote.

Aidha kamanda Mpinga amesema kuwa pia kutakuwa na kamera maalum ambazo zitawekwa barabarani zenye uwezo Wa kutambuwa madereva walioshindwa kulipa faini, makosa ya gari, uhalali Wa leseni, mwendo kasi, kadi na vibali vya gari husika pamoja na kujua kama Dereva amelipa faini au bado.

Afande Mpinga ameongeza kuwa mashine hizi za kielectroniki zitaweka alama za nundu katika leseni zenye makosa na yakifika makosa 15 leseni ya dereva husika itafungiwa kwa miezi 6.