
Taarifa zilizothibitishwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano, Itikadi na uenezi wa CHADEMA, John Mrema amesema kwamba Halima Mdee amefanyiwa upasuaji wa kutolewa uvimbe aliokuwa nao tumboni.
“Amefanyiwa upasuaji alikuwa na uvimbe tumboni. ..yuko Agakhan”, amesema John Mrema.
Hii leo baadhi ya Wabunge wametoa ujumbe wao wa pole kumtakia Mbunge huyo kupona kwa haraka, ili aweze kurejea kwenye majukumu yake ya kawaida.
Mungu akupe nafuu upone haraka pic.twitter.com/OcbLvvXoRN
— ester amos bulaya (@esteramosbulaya) June 8, 2019