
Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Andrea Tsere akiwa katika kijiji Mbugani kata ya Mavanga wilayani humo
Mkuu huyo wa Wilaya pia ameagiza wanachama wa Saccos hiyo kulipa deni la marehemu ambaye alikuwa meneja wa awali aliyefariki kwa kujinyonga mwaka 2012.
Maamuzi hayo yanakuja baada ya kuwepo kwa sintofahamu ya matumizi ya fedha za wanachama na fedha nyingine kulipa hasara iliyosababishwa na marehemu.
Mwenyekiti wa muda wa Saccos hiyo Nasanael Mgani anasema kuwa katiba ya Saccos hiyo ilikiukwa na uongozi wa marehemu na wa sasa kwa kuwa katiba ya chama hicho haikutumika.
Wanachama wa chama hicho wanasema kuwa uamuzi ulio chukuliwa utasaidia kurejeshwa kwa fedha zao.