Sunday , 25th Sep , 2016

Ghasia za siku mbili katika mji wa Jamhuri ya kidemorasi ya Congo zimesababisha vifo vya watu 10.

Vikosi vya usalama Kananga vimekabiliana na wapiganaji wanaotaka kulipiza kisasi mauaji ya kiongozi wao aliyeuawa na jeshi mwezi Agosti, maafisa na vyombo vya habari vinasema.

Wanamgambo hao waliushambulia uwanja wa ndege wa mji huo Ijumaa na kumuua mfanyakazi mmoja wa ndege, walioshuhudia wanasema.

Maandaamano dhidi ya rais Joseph Kabila katika mji mkuu Kinshasa mapema wiki hii yamesababisha vifo vya watu 50, Umoja wa mataifa unasema.