Hakuna maendeleo bila amani na utulivu: Dkt. Shein

Rais Kikwete, mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM ambaye ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Abdulrahman Kinana wakiwa na furaha katika Uwanja wa Demokrasia wa Kibanda Maiti mjini Unguja na kumwaga vipeperushi wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni za chama hicho tawala za kugombea Urais wa Zanzibar Jumapili Septemba 13, 2015
Chama cha mapinduzi CCM leo kimezindua kampeni zake za mgombea urais kupitia chama hicho Dkt. Ally Mohamed shein ambapo wametangaza kupata ushindi wa kishindo kupitia umoja wao.
