Ni kazi sana kukagua wimbo mmoja mmoja -BASATA
Kitendo cha wasanii kutoa wimbo mmoja badala ya albamu iliyokamilika, ni moja ya sababu inayopelekea Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kushindwa kuzipitia na kukagua nyimbo hizo, kwani mfumo uliopo ni wa kukagua albamu iliyokamilika.
Taarifa hiyo imetolewa na Afisa habari wa BASATA Aristide Kwizela, alipokuwa akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio, na kusema kwamba sasa hivi kazi zinazohakikiwa ni zile zilizopo kwenye albam, na kwa upande wa wimbo mmoja mmoja, bado haujawekwa mfumo maalum wa kukagua.