R Kelly kumsaidia mwalimu wake wa muziki

Msanii mkongwe wa muziki wa R&B R. Kelly, amefanya tamasha kubwa katika mji aliotoka wa Chikago, na kuanzisha kampeni ya kukusanya pesa ambazo angemsaidia mwalimu wake wa muziki alipokuwa akisoma.

R. kelly amesema ana deni kwa mwalimu huyo anayeitwa Lena McLin mwenye umri wa miaka 87, kwani ndiye aliyemfikisha alipo sasa kwa kumfundisha muziki, hivyo ameanzisha kampeni hiyo ambayo itamfanya aweze kulipia nyumba yake.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS