Luteni aanza kupasua anga
Rapa mkongwe katika game ya Bongo Flava, Luteni Kalama aliyejijengea jina kubwa kutoka kundi la Gangwe Mobb, ameweka wazi hatua kubwa aliyopiga kimuziki baada ya kupata lebo kutoka nchini Ufaransa, 20K Records ambayo itakuwa ikiendesha kazi zake.