"Hela tunazo" - Rais Magufuli
Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemtaka Balozi wa Marekani afikishe salamu zake kwenye Kampuni ya ndege ya Boeing kuwa wakamilishe haraka ndege ya pili inayotakiwa kufika Tanzania kwa kuwa hela za kulipia zipo.