Mbunge wa Jimbo la Ubungo (CHADEMA), Saed Kubenea, akisalimiana na Rais Dkt. John Magufuli, wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi katika upanuzi wa barabara ya Kimara hadi Kibaha kwa upana wa njia nane na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda.
Mbunge wa Jimbo la Ubungo (CHADEMA), Saed Kubenea amesema kuwa anaunga mkono jitihada zote zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli.