Sita wafariki ajalini Dodoma
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma Dkt. Ernest Ibenzi ameeleza kupokea miili ya watu 6 ambao wamefariki Dunia katika ajali iliyotokea usiku wa kuamkia leo, katika eneo la Kisasa jijini Dodoma, iliyohusisha gari aina ya Toyota Coaster na Lori.

