Wagombea wa Ubunge na Udiwani CCM wapewa onyo
Chama cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Manyoni, Mkoani Singida, kimepiga marufuku watu wote wenye nia ya kugombea nafasi za uongozi katika uchaguzi Mkuu ujao, ikiwemo nafasi ya udiwani na Ubunge, ambao wamekuwa wakivunja kanuni za chama hicho kwa kujipeleka kwa wananchi.

