Muonekano wa mawe baada ya kuvunjwa mithili ya mchanga yaliyotoka kupitia njia ya haja ndogo.
Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imeanza kutoa huduma ya matibabu ya kuvunja mawe kwenye figo na mfumo wa mkojo kwa njia ya mawimbi mshituko kwa kitaalam Extracorporeal shock wave lithotripsy (ESWL).