Jumatano , 31st Jul , 2024

Makamu wa Rais wa Marekani ambaye anapewa kipaumbele na chama chake cha Democratic kuwania urais wa nchi hiyo Kamala Harris ametamani kukutana ana kwa ana na Donald Trump kwenye mjadala wa wazi

Kupitia mitandao ya kijamii Kamala amemtaka Trump kufikiria tena kukutana naye jukwaani huku akisisitiza kuwa kama Trump ana kitu cha kusema basi ni wakati sahihi wa kukisema mbele ya uso wake

Donald Trump alishiriki mdahalo wa kwanza wa wazi dhidi ya aliyekuwa mgombea wa nafasi hiyo Rais Joe Biden ambapo ilionekana wazi Trump kushinda kwa hoja