Alhamisi , 18th Jul , 2024

Kutokana na kuanza kuibuka kwa matukio ya watu kupotea kwa kile kinachodaiwa wanataekwa na watu wasiojulika chama cha Demokrasia na Maendeleo (chadema) Wilaya Kyela Mkoani Mbeya kimewataka wananchi kuchukua taadhari ya kujihami

kwa kumiliki filipi ili wazitumie kutoa taarifa wanapokutwa na mikasa ya kukamatwa na watu wasiyo wafahamu.

Rai hiyo imetolewa na katibu mwenezi wa chama Mtu Gwanongwa sauti ya katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata za Mababu Wilaya Kyela na kuudhuria na Mwenyekiti wa baraza la vijana wa chama hicho BAVICHA John Pambali na katibu mwenyezi Twaa Mwaipaja.

Akizungumza na wananchi waliohudhuria mkutano Mtugwanongwa amesema matukio ya utekaji yalikuwa yamepotea lakini kwa sasa wimbi la ukaji limerejea hivyo ni vema wananchi wakaanza kuchukua taadhari ikiwa ni pamoja na kumiliki filimbi ambayo inmaweza kuwasaidia kupuliza kwa lengo na kutoa taarifa endapo wanakujmbwa na mikasa ya kukamatwa na watu wasiojulika.

Katika Mkutano huo Pambali aliwatka wanannchi wa Wilaya ya Kyela kujitokeza kwa wengi katika zoezi la uboreshaji wa dafatri la wapika kura ili kuweza kushirika vyema uchaguzi wa viongozi wa Serikali za mitaa ambayo unatarajiwa kufika mwishoni mwa mwaka huu.

Pambalu amesema njia ya pekee ya kuondokana na mateso wanayoyapaya ya maisha magumu ni kushirika vyema katika kujioandikisha lakini pia wajitokeza katika uchaguzi wa serikali za mitaa ili kupata viongozi ambao wanapambania.