Jumatano , 25th Oct , 2023

The Biggest Boss Rick Ross amefunguka kuwa yupo tayari kukataa na kuacha mkwanja wa Tsh Bilioni 1 ili kupata Dinner moja na Jay Z kwa sababu ya kutaka kujifunza na kupata maarifa kutoka kwa Jay Z.

Picha ya Rick Ross kulia na Jay Z kushoto

Rick Ross amesema atachagua Dinner na Jay Z kwa sababu alipata bahati ya kula naye Lunch kabla hajaachia Album yake ya pili na alimshauri mambo mengi ya kimuziki kufika level za mbali na kumpa madini ya maisha kufanikiwa zaidi.

Rozay ameongeza kusema hata ikitokea ameambiwa tena kuchagua Dinner au kupewa Tsh Bilioni 1 yeye atachugua kukaa meza moja na Jay Z ili kujifunza zaidi na kupata maarifa.