Jumatatu , 23rd Oct , 2023

Siku kama ya leo miaka 83 iliyopita mmoja wa wachezaji wakubwa kuwahi kutokea katika historia ya mpira wa miguu Edson Arantes do Nascimento Maarufu kama PELE alizaliwa na hii leo angekuwa anatimiza umri wa miaka 83.

Miongoni mwa rekodi anazoendelea kushikilia Pele hadi hivi sasa ni rekodi ya kuwa mchezaji pekee duniani aliyewahi kushinda kombe la dunia akiwa na umri mdogo zaidi ambapo alikuwa na umri wa miaka 17 tu mnamo mwaka 1958. Na pia ndiye binadamu pekee aliyefanikiwa kushinda vikombe vitatu vya kombe la dunia alishinda mwaka 1958, 1962 na mwaka 1970.