
Balozi wa Tanzania nchini Israel, Alex Kallua
Balozi wa Tanzania nchini Israel, Alex Kallua, amesema mpaka asubuhi ya leo Oktoba 9, 2023, ubalozi huo umekuwa na mawasiliano na Watanzania takribani 350 waliopo nchini humo kasoro wanafunzi hao wawili.
"Tunaendelea kuwafuatilia Watanzania wawili ambao ni wanafunzi waliokuwa wanafanya mafunzo kwa vitendo kusini mwa nchi hiyo, tunafanya jitihada za kuwapata kwanza ili kufahamu walipo na hali zao," amesema Balozi Alex