Jumanne , 3rd Oct , 2023

Kikosi cha JKT Tanzania kimeondoka na alama tatu katika uwanja wake wa nyumbani wa CCM Kambarage mkoani Shinyaga baada ya kupata ushindi wa bao 1- 0 dhidi ya watani wao wa jadi Mashujaa FC ya mkoani Kigoma.

Bao pekee la JKT Tanzania Limefungwa na Edward Songo  katika kipindi cha pili cha mchezo na ushindi huu unakuwa ni kwanza kwa kikosi hicho katika michezo yake ambayo imeshuka dimbani.

Baada ya ushindi huo kikosi hicho cha JKT Tanzania kinachofundishwa na kocha Malale Hamisi kimesogea hadi nafasi ya saba kikiwa na alama zake tano katika michezo mitano ambayo imeshuka dimbani.