
Wananchi pamoja na Askari wakichimba msingi
Wakazi hao wameeleza kuwa hatua hiyo imekuja baada ya Tarafa hiyo yenye jumla ya Kata 6, vijiji 30 na vitongoji 223 kukosa kituo cha polisi suala linalofanya kuwepo kwa uhalifu na kuwafanya kukosa usalama.
Akizungumza na wananchi hao Mkuu wa wilaya ya Kwimba Ng'wilabuzu Ludigija, amewapongeza kwa hatua hiyo akisema kujengwa kwa kituo hicho kutafungua fursa za uwekezaji katika maeneo hayo.