Jumapili , 11th Dec , 2022

Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade)Latifa Khamis amesema kuwa kuwa kuanzia sasa serikali itafanya kazi na Chama Cha Vipidozi Tanzania (TCA) ikiwa ni katika kuhakikisha wanalinda afya za watumiaji wa vipodozi na sekta ya urembo na watanzania wote kwa ujumla

Mkurugenzi Mkuu, Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade)Latifa Khamis

Mkurugenzi huyo amesema hayo wakati alipokuwa mgeni rasmi katika uzinduzi Tamasha la siku moja 'Vipodozi Day' lililofanyika kwenye viwanja vya Leaders Club Kinondoni Jijini Dar es Salaam akimwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji.

Amesema enzi za kupenda na kithamini vipodozi au bidhaa kutoka nje ya nchi zimepitwa na wakati. Hivyo nifursa sasa kutumia jukwaa hilo kuongeza kasi katika uzalishaji wa vipodozi visivyo na viambata vyenye akiwaahidi kuwa Tantrade itawapa fursa ya kujitangaza kitaifa na kimataifa.